Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 21:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.

Gade chapit la Kopi




Mezali 21:2
18 Referans Kwoze  

Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.


Kuna njia mutu anayoona kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Musijidanganye ninyi wenyewe kwa kusikiliza tu neno la Mungu, lakini mulitimize kwa matendo.


Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake.


Kama mutu akijizania kwamba yeye ni kitu, ijapokuwa yeye si kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.


Watu wengi wanajivunia kuwa wema, lakini mwaminifu wa kweli anapatikana wapi?


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


TEKELI: wewe umepimwa kwenye mizani, nawe ukaonekana hauna uzito wowote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite