10 Mutu mwovu anatamani kutenda uovu; hata kwa jirani yake hana huruma.
Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.
Usipange maovu juu ya jirani yako anayeishi karibu nawe bila wasiwasi.
Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.
Mambo hayo ni mufano kwetu, kusudi tusikuwe na tamaa mbaya kama vile wao.
Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.
Matumaini ya waovu yanaporomoka na kuharibika, lakini mutu mwenye haki anasimama imara.
Anatoa kwa moyo safi, anawapa wamasikini. Haki yake inadumu milele. Ana nguvu na sifa.
Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.
Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema.
watu wanaofurahia kutenda maovu na kupendezwa na upotovu wa maovu,
Anayemuzarau jirani yake ni mwenye zambi, lakini ana heri yule anayekuwa mwema kwa masikini.
Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.