8 Mufalme anapoikaa kwa kutoa hukumu, anapepeta uovu wote kwa macho yake.
Uwaondoe waovu mbele ya mufalme, na utawala wake utaimarika katika haki.
Mufalme mwenye hekima anapepeta waovu; anawaazibu bila huruma.
Mufalme anayewaamua wamasikini kwa haki, ataona utawala wake unaimarika milele.
Ee mufalme mukubwa, mupenda haki, umesimamisha usawa katika Israeli; umeleta sheria na haki.
Kutatokea mufalme atakayetawala kwa haki, nao wakubwa wataongoza kwa kufuatana na sheria ya Mungu.
Ni chukizo kubwa kwa wafalme kutenda uovu, maana musingi wa mamlaka yao ni haki.
Lakini wewe, ee Yawe, ni mukubwa kwa milele.
Mufalme awatetee wamasikini wa taifa, awasaidie wakosefu, na kuwaangamiza watesaji.
yeye ni kama mwangaza wa asubui, jua linapochomoza asubui isiyokuwa na mawingu. Yeye ni kama mvua inayootesha majani juu ya udongo.
“Asiyekuwa wa upande wangu ni adui yangu; na asiyekusanya pamoja nami, anasambaza.
Solomono alijenga uwanja wa kiti cha kifalme ambamo aliamulia maneno ya watu. Huu uliitwa vilevile Uwanja wa Hukumu. Ulipambwa kwa mbao za mierezi kutoka sakafu mpaka dari.