Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 20:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mali iliyopatikana kwa haraka kwa mwanzo, haitakuwa ya heri kwa mwisho.

Gade chapit la Kopi




Mezali 20:21
13 Referans Kwoze  

Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.


Lakini wale wanaotaka kuwa watajiri wanaanguka katika majaribu na mitego, na katika tamaa nyingi za upumbafu na mabaya zinazowatumbukiza katika anguko na uharibifu.


Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo na kumutungia misemo ya kitambi: Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako, na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi! Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?


Mutu muchoyo anakimbilia mali, wala hajui kwamba ukosefu utamufikia.


Mutu mwaminifu atapata baraka tele, lakini mwenye pupa ya kuwa tajiri hataepuka azabu.


Anayeongeza mali yake kwa mazidio na kulipisha faida, anamukusanyia mwingine mwenye kuwahurumia wamasikini.


Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.


Anayemulaani baba yake au mama yake, mwangaza wa uzima wake utazimika kama taa katika giza.


Usiseme: “Nitalipiza ubaya niliotendewa.” Umutegemee Yawe naye atakusaidia.


Mali inayopatikana kwa udanganyifu ni muvuke unaopita na mutego wa kifo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite