Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 2:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Maana Yawe anawapa watu hekima; katika kinywa chake kunatoka maarifa na ufahamu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 2:6
32 Referans Kwoze  

Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.


Amri yako iko nami siku zote, inanipa hekima kuliko waadui zangu.


Lakini ile roho inayokuwa ndani ya mutu, ile pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo, ndiyo inayomwezesha mwanadamu kufahamu.


Kwa maana mimi mwenyewe nitawapa masemi na hekima hata waadui zenu hawataweza kuyapinga wala kuyakataa.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Imeandikwa hivi katika maandiko ya manabii: ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Kila mutu anayemusikia Baba na kufuata mafundisho yake, anakuja kwangu.


basi, sasa ninakutimizia kama ulivyoomba. Ninakupa hekima na akili kwa kipimo ambacho hakuna mutu mwingine aliyepata kuwa nacho mbele yako, na wala hakutatokea mwingine kama wewe nyuma yako.


Kila zawadi nzuri na kila zawadi kamilifu inatoka juu kwa Mungu Baba aliyeumba miangaza yote inayokuwa katika mbingu. Mungu hawezi kubadilika wala kugeuka.


Kwa kanuni zako ninapata hekima, kwa hiyo ninachukia kila mwenendo mubaya.


Kwako, ee Mungu wa babu zangu, ninatoa shukrani na kukusifu, maana umenipa hekima na nguvu, umetujulisha kile tulichokuomba, umetujulisha yale maneno ya mufalme.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.


Anabadilisha nyakati na wakati, anaondoa na kuwatawalisha wafalme. Anawapa hekima wenye hekima, anawaongezea wenye maarifa ufahamu.


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


Linatokea kwa upande mumoja, na kuzunguka mpaka upande mwingine; hakuna kinachoweza kuepuka joto lake.


Kwa hiyo, ninakuomba unipe mimi mutumishi wako moyo wa hekima nipate kuamua watu wako, niweze kutambua mazuri na mabaya; maana ni nani anayeweza kuhukumu watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


na kumujaza Roho wangu. Nimemupatia ufahamu na akili, maarifa na ufundi,


Yawe akupe hekima na akili kusudi atakapokupa uongozi juu ya Israeli, ushike sheria za Yawe, Mungu wako.


Mungu akanipa moyo kuwakusanya viongozi na watu kwa kujua ukoo zao. Nikapata kitabu cha ukoo za watu waliorudi toka katika uhamisho mara ya kwanza, na hawa ndio waliokuwa wameandikwa ndani yake.


Pokea mafundisho kutoka kwake; na uyaweke maneno yake ndani ya moyo wako.


Nimekukosea wewe peke yako, nimetenda mabaya mbele yako. Hivi uamuzi wako ni wa haki, hukumu yako haipotoki.


Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.


Watu wa inchi zote walikuwa na hamu ya kumwendea Solomono kwa kusikiliza hekima yake ambayo Mungu alikuwa amemujalia.


Nawe Ezra, kwa kutumia hekima Mungu wako aliyokupa, hiyo unayokuwa nayo, chagua wanasheria, na waamuzi watakaowaongoza wakaaji wote wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati ambao wanaishi kufuatana na Sheria ya Mungu wako. Na yule ambaye haijui Sheria hiyo, umufundishe.


Lakini hekima na uwezo ni vya Mungu. Yeye ana maarifa na ujuzi.


Yeye ana nguvu na hekima. Wanaodanganywa na wanaodanganya ni wake.


Sheria ya Yawe ni kamilifu; inamupa mutu uzima mupya. Maagizo ya Yawe ni ya kuaminiwa; yanawapa wajinga hekima.


Mwenye kuonya mataifa, yeye hawezi kuazibu? Mwenye kufundisha wanadamu, yeye hana akili?


Unieleweshe nipate kushika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite