3 ukiomba upewe akili, ukisihi upewe ufahamu,
Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.
Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.
Kilio changu kikufikie, ee Yawe! Unijalie akili kama ulivyoahidi.
Mimi ni mutumishi wako. Unipe akili nipate kujua maagizo yako.
Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, inaonyesha hakika kwamba Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa Roho Mutakatifu wale wanaomwomba kwake.”
Kwa mikono yako wewe mwenyewe uliniumba; unijalie akili nijifunze amri zako.
Unieleweshe nipate kushika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote.
Yawe akupe hekima na akili kusudi atakapokupa uongozi juu ya Israeli, ushike sheria za Yawe, Mungu wako.
Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.
ukitega sikio lako kwa kusikiliza hekima, na kuelekeza moyo wako upate ufahamu,
ukitafuta hekima kama feza, na kuitaka kama hazina iliyofichwa,
Wana wangu, musikilize maadibisho ya baba yenu, mutege sikio mupate kuwa na akili.