15 watu ambao mienendo yao imepotoka, nazo njia zao haziaminiki.
Lakini wanaogeuka na kufuata njia zao mbaya, uwatoweshe pamoja na watenda maovu. Amani ikuwe na Israeli!
Njia ya mutu mwenye kosa imepotoka, lakini mwenendo wa mwenye moyo safi ni sawa.
kusudi mupate kuwa bila kosa na kuwa na maisha safi. Hivi mutakuwa watoto wakamilifu wa Mungu wasiokuwa na kilema kati ya watu waovu na wapotovu wa dunia hii. Munapaswa kuangaza kati ya watu hawa kama vile nyota zinavyoangaza katika mbingu,
Lakini ninyi mumekosa uaminifu kwake, ninyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu, ninyi ni kizazi kiovu na kipotovu.
Njia ya amani hamuijui hata kidogo; hamufuati sheria ya Mungu. Mumejifanyia njia potovu, yeyote anayepitia humo hapati amani.
Kinywa changu kitasema maneno ya haki, hakuna udanganyifu wala upotevu katika midomo yangu.
Mwenye mwenendo sawa anamwogopa Yawe, lakini mupotovu anamuzarau Mungu.