12 vitakuepusha na njia ya uovu, na watu wa maneno mapotovu,
Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”
Anayeandamana na wenye hekima anapata hekima, lakini anayejiunga na wapumbafu atapata hasara.
Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.
Kwa sababu hiyo Bwana anasema: “Mutoke kati yao, mujitenge nao. Musiguse kitu chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu, nami nitawapokea.
Na hata kati yenu kutatokea watu watakaotoa mafundisho ya kupotosha wengine kusudi wawavute waamini kuwafuata.
Achana na ujinga upate kuishi; fuata njia ya akili.”
Maana waovu ni chukizo kwa Yawe, yeye anawafanya watu wa usawa kuwa warafiki zake.
Unikinge nisielekee kufanya mabaya, nisijishugulishe na matendo maovu, nisijiunge na watu wanaotenda mabaya, wala nisishiriki hata kidogo katika karamu zao.
Upotovu wowote ukuwe mbali nami; sitahusika kabisa na uovu.
Mutu mwovu, mutu asiyefaa kitu, anatangatanga akisema maneno mapotovu.
Midomo ya wenye haki inajua mambo yatakayokubaliwa, lakini vinywa vya waovu vinasema tu maovu.
Macho yako yataona mambo ya ajabu, moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mupumbafu; lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.