7 Masikini anachukiwa na wandugu zake; warafiki zake ndio zaidi: wanamukimbia! Hata awabembeleze namna gani, hatawapata.
Mali inavuta warafiki wengi wapya, lakini masikini anaachwa na rafiki yake.
Anayekataa kusikia kilio cha masikini hatasikilizwa atakapolilia musaada.
Masikini anaomba kwa unyenyekevu, lakini tajiri anajibu kwa ukali.
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zimeniishia; hata macho yangu nayo yamekwisha fifia.
Lakini ninyi munawazarau wamasikini! Watajiri si ndio wale wanaowagandamiza ninyi na kuwashitaki kwenye tribinali?
Masikini anachukiwa hata na jirani yake, lakini tajiri ana warafiki wengi.
Yananizunguka kama mafuriko muchana kutwa; yananizunguka yote pamoja.
Hasira yako imenilemea; umenisonga kwa zoruba yako yote.
Mali ya tajiri ndiyo kikingio chake. Umasikini wa masikini unamuletea maangamizi.
Warafiki na wenzangu wanaepuka kuona mateso yangu, na wandugu zangu wanakaa mbali nami.
Usisahau warafiki zako wala wa baba yako. Ukipatwa na magumu usikimbilie kwa ndugu yako. Afazali jirani ambaye iko karibu kuliko ndugu anayekuwa mbali.