7 Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe.
Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Ee Yawe, usiwape waovu vitu wanavyotaka, wala mipango yao mibaya usiifanikishe.
Lakini Mungu atawapiga mishale, na kuwaumiza kwa rafla.
ikiwa umejifunga kwa maneno yako mwenyewe, utajinasa kwa ahadi uliyofanya;
Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
Yefuta alipomwona, akapasua nguo yake kwa huzuni na kusema: “Ee binti yangu! Umenivunja moyo. Wewe umekuwa chanzo kikubwa cha matatizo kwangu. Nimekwisha kumwapia Yawe nami siwezi kuvunja kiapo changu.”
Maneno ya muchongeaji ni kama chakula kitamu ambacho kinashuka mpaka ndani kabisa ya tumbo.
Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.
Hekima ni chemichemi ya uzima kwa yule anayekuwa nayo, lakini upumbafu ni azabu ya wapumbafu.