6 Maneno ya mupumbafu yanaleta ugomvi; kila neno analosema linasababisha azabu.
Jiwe ni zito na muchanga vilevile, lakini uchokozi wa mupumbafu ni muzito zaidi.
Mwenye hekima akibishana na mupumbafu, akasirike au acheke, ni mamoja; hatatulia.
Afazali kuishi pembeni juu ya paa, kuliko kuishi ndani ya nyumba pamoja na mwanamuke mugomvi.
Ni jambo la heshima kuepuka ugomvi; wapumbafu ndio wanaogombana.
Azabu iko tayari kwa wenye kuzarau, na mapigo kwa migongo ya wapumbafu.
Mutu wa hasira kali anapaswa kupata azabu; ukimwachilia mara moja itakuomba kumwachilia tena.
Kuanzisha ugomvi ni kama kufungua maji ya kisima; achana na ugomvi mbele haujafurika.
Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.
Kiburi kinasababisha tu ugomvi, lakini kwa wanaokubali shauri jema kuna hekima.
Ujinga wa mupumbafu unajulikana mara moja, lakini mwerevu anazarau matusi.
Umufukuze mwenye kiburi na fujo itatoweka, na ugomvi na matusi vitakoma.