Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 18:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki.

Gade chapit la Kopi




Mezali 18:5
20 Referans Kwoze  

Unapotoa hukumu uamue kwa haki, usimupendelee masikini wala kumwogopa mwenye cheo. Lakini hukumu mwenzako kwa haki.


Si vizuri kumubagua mutu. Watu wanafanya mabaya hata kwa ajili ya mukate.


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


“Mpaka wakati gani mutaendelea kuhukumu bila haki na kuwapendelea watu waovu?


Hii ni misemo mingine ya wenye hekima. Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.


Kumuhesabu mwovu kuwa na haki na kumwazibu asiyekuwa na kosa, yote mawili ni chukizo kwa Yawe.


Halafu wakatuma kwake wamoja kati ya wanafunzi wao pamoja na watu wengine wamoja waliojiunga na Herode kumwuliza maneno haya: “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mutu wa kweli na kwamba unafundisha kwa kweli njia Mungu anayoamuru. Vilevile haushuguliki na mafikiri ya mutu yeyote kwa sababu hauangalii cheo cha mutu.


Kwa ajili ya kituliro kidogo wanawaachilia wenye kosa na kuwanyima wasiokuwa na kosa haki yao.


Yeye hawapendelei wakubwa, wala kuwajali watajiri kuliko wamasikini, maana wote hao ni kazi ya mikono yake.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Sheria ya Mungu imewekwa pembeni, haki iko mbali; ukweli unakanyagwa katika tribinali, usawa hauwezi kuingia humo.


Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.


Usipotoshe haki masikini anayostahili katika mashitaki yake.


Si vizuri kumwazibu mutu asiyekuwa na kosa; ni kosa kuwapiga fimbo wenye heshima.


Wakikunywa watasahau maagizo ya sheria, na kuwanyima haki wenye taabu.


Musikie jambo hili, enyi waongozi wa wazao wa Yakobo, musikilize, enyi watawala wa Waisraeli: Ninyi munachukia sheria ya Mungu na kupotosha mambo ya usawa.


Usikuwe na upendeleo katika mashitaki ya masikini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite