3 Mwovu anapokuja, mazarau yanakuja vilevile; pamoja na haya, matusi yanakuja.
Umufukuze mwenye kiburi na fujo itatoweka, na ugomvi na matusi vitakoma.
Ninyi ni wenye heri kama watu wakiwatukana kwa ajili ya Kristo, kwa kuwa Roho wa utukufu, maana yake Roho wa Mungu anakaa ndani yenu.
Waovu wakiongozeka, zambi zinaongezeka. Lakini wenye haki watashuhudia kuanguka kwao.
Kiburi kinazaa haya, lakini kwa watu wanyenyekevu kuna hekima.
Sasa, wapagani wanashangaa kuona ninyi hamushirikiani nao tena katika maisha ya ovyo ovyo; na kwa hiyo wanawasingizia ninyi.
Wewe unajua ninavyotukanwa, unajua haya na matusi ninazopata; na waadui zangu wote wewe unawajua.
Nimekuwa mugeni kwa wandugu zangu, kaka na dada zangu hawanitambui.
Watu wa Yuda wakakuwa wanalalamika wakisema: “Tunachoka na kubeba mizigo na bado kuna takataka nyingi za kubeba. Hatuwezi kuendelea kujenga ukuta.”
Kwa hiyo Saulo akawaka hasira juu ya Yonatani, akamwambia: “Mwana wa imbwa wewe! Ninajua kwamba umejichagulia mwana wa Yese kwa ajili ya haya yako mwenyewe, na kumufezehesha mama yako!
Mupumbafu hapendezwi na ufahamu; kitu cha maana kwake ni maoni yake tu.
Maneno ya kinywa cha mutu ni kilindi cha maji; chemichemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
Mwenye haki anachukia uongo, lakini mwovu anatenda kwa kupatisha haya na mazarau.