Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.
Yakobo akamwambia: “Hapana! Kama kweli nimekubaliwa mbele yako, ninakusihi uipokee zawadi yangu. Hakika, kuona uso wako ni kama kuona uso wa Mungu, kwa vile ulivyonipokea kwa wema mukubwa.
Mufalme wa Aramu akamwambia: “Twaa barua hii umupelekee mufalme wa Israeli.” Hivyo Namani akaondoka, akipeleka vikoroti elfu makumi tatu vya feza, vikoroti elfu sita vya zahabu na nguo kumi za sikukuu.