9 Anayesamehe makosa anajenga urafiki, lakini anayekumbusha makosa anatenga warafiki.
Chuki inaleta ugomvi, lakini upendo unafunika makosa yote.
Na zaidi ya yote mudumu katika upendo ninyi kwa ninyi, maana upendo unafunika zambi nyingi.
Mutu mupotovu anatawanya ugomvi, na muchonganishi anatenganisha warafiki.
Zaburi ya Daudi: Mashairi. Heri mutu aliyesamehewa kosa lake, mutu ambaye zambi yake imeondolewa kabisa.
Upendo unavumilia, ni wenye wema; upendo hauna wivu, upendo haujivuni, na hauna kiburi.
mukumbuke neno hili: yule anayemurudisha mwenye zambi toka njia ya upotevu ataokoa roho ya yule kutoka kifo, na zambi nyingi zitasamehewa.
Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.