7 Maneno mazuri hayastahili katika kinywa cha mupumbafu, zaidi sana maneno ya uongo katika kinywa cha kiongozi!
Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.
Wewe munafiki, ondosha kwanza nguzo kutoka ndani ya jicho lako, kisha utaweza kuona waziwazi na kuweza kuondoa ile vumbi inayokuwa ndani ya jicho la ndugu yako.
Mezali katika midomo ya mupumbafu ni kama miguu ya kiwete inayoninginia.
Ukweli unadumu milele, lakini uongo ni wa muda kidogo tu.
Ni ukweli mutupu: Mungu hafanyi jambo ovu. Mungu Mwenye Uwezo hapotoshi haki hata kidogo.
Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,
Usiniache nifezeheke, ee Yawe, maana mimi ninakulilia; lakini uwaache waovu wafezeheke, uwaache wapotelee huko kuzimu.
Macho ya kiburi, ulimi mudanganyifu, mikono inayoua wasiokuwa na kosa,
Kinywa kinachosema uongo ni chukizo kwa Yawe, lakini watu waaminifu ni furaha yake.
Haifai kwa mupumbafu kuishi kwa raha; tena ni vibaya zaidi mutumwa kuwatawala wakubwa.
Kwa mupumbafu hekima ni ngumu kuielewa; penye mukutano wa mashauri hafungui mudomo.
Heshima anayopewa mupumbafu haifai. Ni kama teluji ya wakati wa kipwa, au mvua ya wakati wa mavuno.