10 Onyo kwa mwenye akili lina maana, kuliko mapigo mia moja kwa mupumbafu.
Mimi ninawaonya na kuwaazibu wote ninaowapenda. Basi ufanye nguvu, ugeuke toka katika zambi.
Mutumwa haonyeki kwa maneno matupu; maana ingawa anayaelewa, yeye hatayatii.
Hata kama ukitwanga mupumbafu katika kinu, sawa na ngano, hautaweza kumutenganisha na upumbafu wake.
Umwazibu mwenye kuzarau naye mujinga atapata akili; umwonye mwenye akili naye atapata maarifa.
Mupumbafu anazarau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ni mwenye akili.
Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.
Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.
Anayesamehe makosa anajenga urafiki, lakini anayekumbusha makosa anatenga warafiki.
Nia ya mutu mwovu ni kuasi tu; mujumbe mubaya atatumwa juu yake.