Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 16:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.

Gade chapit la Kopi




Mezali 16:7
24 Referans Kwoze  

Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Nasi tunapokea jambo lolote tunaloomba kwake, kwa sababu tunatii amri zake na kutenda mambo yanayomupendeza.


Hivi, mutaweza kuishi sawa Bwana anavyotaka na kumupendeza katika mambo yote. Kwa njia hiyo mutafikia kufanya matendo mema ya kila namna na kuzidi kumujua Mungu.


Yawe akaogopesha falme zote jirani za inchi ya Yuda, zikaogopa kupigana vita na Yosafati.


awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.


Basi, ee Yawe, acha laana hizo zinipate kama sikukutumikia vizuri na kama sikukusihi kwa ajili ya waadui zangu wakati walipokuwa katika taabu na shida!


Basi, Esau akakwenda mbio kumupokea Yakobo, akamukumbatia, kumubusu kwenye shingo, na wote wawili wakalia.


Naye akamwuliza: “Jina lako nani?” Yeye akamujibu: “Yakobo.”


Watoto muwatii wazazi wenu katika mambo yote, kwa maana jambo hili linamupendeza Bwana.


Kweli nina vitu vyote vya lazima na zaidi kupita. Sasa kwa kuwa Epafrodito ameniletea zawadi zenu zote, ninatosheka. Zawadi hizi ni kama sadaka ya ubani yenye harufu nzuri, na kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto inayokubaliwa na Mungu na kumupendeza.


Kwa wimbo nitalisifu jina la Mungu, nitamutukuza kwa shukrani.


Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”


Ni nani atakayewazuru ninyi kama mukiwa wenye bidii katika kutenda mema?


“Tena nitafanya Waisraeli wapate kukubaliwa mbele ya Wamisri na mutakapoondoka Misri, hamutatoka mikono mitupu.


Njia zake ni za kupendeza, zote zinaelekea kwenye amani.


Afazali mali kidogo kwa njia ya haki, kuliko mapato mengi kwa njia isiyofuatana na sheria ya Mungu.


Umutwae Yeremia, umutunze vema wala usimuzuru; umutendee kama anavyokuambia.


Nitawahurumia na kumufanya mufalme awahurumie na kuwaacha katika inchi yenu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Basi, Mungu akamujalia Danieli kupendelewa na kuhurumiwa na Aspenazi, yule mukubwa.


Basi, Yosafati akatawala kwa amani, na Mungu akamupa amani pande zote.


Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite