3 Tegemea Yawe katika kazi yako, nayo mipango yako itafanikiwa.
Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.
Maneno yake ni matamu kuliko maziwa, lakini mawazo yake ni ya kufanya vita. Maneno yake ni laini kama mafuta, lakini yanakata kama upanga mukali.
Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.
Mumutolee masumbuko yenu yote kwa maana yeye anawashugulikia.
Kwa ngambo yangu, mimi ningemugeukia Mungu, ningemutolea Mungu maneno yangu,
Neno lolote utakalokusudia litafanikiwa, na mwangaza utaangazia njia zako.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Ni kwa sababu hii ninawaambia: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwamba mutakula nini; wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu, kwamba mutavaa nini.