Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 16:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Mwenye hekima ndani ya moyo anaitwa mwenye akili; neno la kupendeza linawavuta watu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 16:21
18 Referans Kwoze  

Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.


Mafuta na marasi vinafurahisha moyo, vilevile utamu wa urafiki kuliko kujitoshelea mwenyewe.


Lakini hekima inayotoka mbinguni, kwanza ni safi, tena ni yenye amani, upole na usikilivu, inajaa huruma na matendo mema. Haina upendeleo wala udanganyifu.


Walinzi wakajibu: “Hatujasikia mutu akisema sawasawa na mutu yule!”


Nao wote wakamufurahia na kushangaa na maneno mazuri aliyosema. Wakasema: “Huyu si mwana wa Yosefu?”


Muhubiri alijikaza kupata maneno ya kupendeza, akaandika kwa usawa maneno ya kweli.


Mwana wangu, moyo wako ukiwa wenye hekima, moyo wangu vilevile utakuwa wenye furaha.


Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.


Moyo wangu umejaa mawazo mazuri: ninamutungia mufalme mashairi yangu, ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi hodari.


basi, sasa ninakutimizia kama ulivyoomba. Ninakupa hekima na akili kwa kipimo ambacho hakuna mutu mwingine aliyepata kuwa nacho mbele yako, na wala hakutatokea mwingine kama wewe nyuma yako.


Watu wote wanajua namna munavyomutii Bwana, na kwa sababu hii ninafurahi kwa ajili yenu. Lakini ninataka mukuwe wenye hekima kwa kutenda mema, na mukuwe safi mukijitenga na mambo mabaya.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Hekima ni chemichemi ya uzima kwa yule anayekuwa nayo, lakini upumbafu ni azabu ya wapumbafu.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Katika kinywa cha mwenye ufahamu kuna hekima, lakini wasiokuwa na akili watapigwa fimbo katika mugongo.


Kwa mupumbafu, kutenda maovu ni kama muchezo, lakini watu wenye akili wanafurahia hekima.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite