Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 16:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Matendo yote ya mutu yanaonekana kwake kuwa sawa lakini Yawe anapima nia ya mutu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 16:2
23 Referans Kwoze  

Matendo yote ya mutu ni sawa katika macho yake, lakini Yawe anapima mioyo.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


Yesu akawaambia: “Ninyi ni watu wanaojionyesha kuwa wenye haki mbele ya watu, lakini Mungu anajua yanayokuwa ndani ya mioyo yenu. Kwa maana mambo yanayosifiwa na watu ni machukizo mbele ya Mungu.


Kuna watu ambao wanajiona kuwa safi, kumbe bado hawajatakaswa uchafu wao.


Mimi Yawe ninapima akili na kuchunguza moyo wa mutu. Na hivyo ninamutendea kila mumoja, kulingana na mwenendo wake, kadiri ya matendo yake.


Usiseme kisha: “Hatukujua!” Maana Mungu anayepima mioyo ya watu anaona; yeye atakulipa kulingana na matendo yako!


Zambi inaongea na mutu mwovu, ndani kabisa ya moyo wake; kuogopa Mungu si kitu kwake.


Maana mwenendo wa kila mutu ni wazi mbele ya Yawe; yeye anachunguza njia zake zote.


Kuna njia mutu anayoona kuwa sawa, lakini kwa mwisho inaongoza kwenye kifo.


TEKELI: wewe umepimwa kwenye mizani, nawe ukaonekana hauna uzito wowote.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Nitawaua wafuasi wake. Na hivi makanisa yote yatajua kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo ya watu na mafikiri yao. Vilevile yatajua kwamba mimi nitamulipa kila mumoja wenu kufuatana na matendo yake.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Tuatera hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa Mwana wa Mungu, anayekuwa na macho yanayometameta kama ndimi za moto, na miguu inayongaa kama shaba iliyosafishwa vizuri sana.


Muache kujisifu, muache kusema kwa kiburi. Maana anayejua ni Yawe. Yeye anayapima matendo yote.


Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.


Malaika wa Yawe akamwambia Balamu: Mbona umemupiga punda wako mara tatu? Nimekuja kukuzuia, kwa sababu njia yako ni mbaya.


Jumla ya waliokunywa maji kwa kuchota kwa mikono yao na kulamba kama imbwa ilikuwa mia tatu. Lakini wengine wote waliobaki walipiga magoti kwa kunywa maji.


Siku hizo hakukukuwa mufalme katika Israeli. Kila mutu alifanya chochote alichotaka.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite