Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 15:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mwenendo wa waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini Mungu anawapenda wale wanaofuata mambo ya haki.

Gade chapit la Kopi




Mezali 15:9
21 Referans Kwoze  

Lakini wewe mutu wa Mungu, uepuke mambo haya, ushikamane na haki, ibada, imani, upendo, uvumilivu na upole.


Anayetafuta haki na wema atapata uzima, haki, na heshima.


“Muingie kwa kupitia mulango unaokuwa mwembamba. Kwa maana njia inayoongoza kufikia kwenye lufu ni kubwa, nao mulango unaoiingilia ni mupana, nao watu wanaoipitia ni wengi.


Wewe ni mutakatifu kabisa, hauwezi kutazama uovu, hauwezi kuvumilia hata kidogo kuona mabaya. Mbona basi unawaona wafanya maovu na kunyamaza, kwa nini unanyamaza waovu wanapowamaliza wale watu wanaokuwa wenye haki kuliko wao?


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Hata hivyo, mimi niliwatuma kwenu siku zote watumishi wangu manabii nikisema: Musifanye jambo hili baya ninalolichukia!


Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Munisikilize, enyi munaojua mambo ya haki, ambao sheria zangu ziko ndani ya mioyo yenu. Musiogope mazarau ya watu, wala kufazaishwa na masimango yao.


Yawe anasema hivi: Munisikilize enyi munaotaka kukombolewa, ninyi munaonitafuta mimi Yawe. Muangalie jiwe mulilochongwa toka ndani yake, mulima mulimochimbuliwa.


Njia ya watu wa haki ni yenye kunyooka; ewe Mungu mwenye haki, unasawanisha njia yao.


Njia ya mutu mwenye kosa imepotoka, lakini mwenendo wa mwenye moyo safi ni sawa.


Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.


Lakini njia ya waovu ni kama giza nene, hawajui kinachowafanya wajikwae.


Maana Yawe anashugulikia njia ya watu wa haki; lakini njia ya waovu itaangamia.


Atawapenda na kuwabariki, nanyi mutaongezeka na kuwa na wazao wengi. Atabariki mashamba yenu kusudi mupate ngano, divai na mafuta. Atawabariki kwa kuwapa ngombe na kondoo wengi katika inchi aliyowaahidi babu zenu kwamba atawapa ninyi.


Uangalie kama mwenendo wangu ni mubaya, uniongoze katika njia ya milele.


Kumwogopa Yawe ni kuchukia uovu. Ninachukia kiburi, majivuno maisha mabaya, na luga mbaya.


Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.


Wewe si Mungu anayependa ubaya; mwovu hawezi kupokelewa kwako.


Yawe ni wa haki na anapenda watu watende kwa haki. Watu wa usawa wataona uso wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite