6 Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.
Kama mumoja kati yenu akikosa kuwa na hekima, aiombe kwa Mungu ambaye atamupatia. Kwa maana Mungu anawapa watu wote bila upendeleo na kwa moyo mwema.
Kama mutu anajizania kwamba anajua kitu, yeye hakijui hakika sawa vile inavyomupasa kukijua.
Kwa mutu mwenye ufahamu kila kitu ni wazi, kwa mwenye maarifa yote imesawanishwa.
Wenye hekima kati yenu wanafezeheka, watahangaishwa na kunaswa. Wamelikataa neno la Yawe. Basi ni hekima gani wanayokuwa nayo?
Hakika anayesema hivyo hajapata kuona mwangaza. Lakini ninyi mushike lile agizo na mafundisho ya Mungu.
Unamwona mutu anayejiona kuwa mwenye hekima? Afazali kumutumainia mupumbafu kuliko yule.
Mupumbafu hapendezwi na ufahamu; kitu cha maana kwake ni maoni yake tu.
Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.
Uyafungue macho yangu, nipate kuona maajabu ya sheria yako.
Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.
Mushuhuda mwaminifu hasemi uongo, lakini asiyeaminiwa anabubujika uongo.
Ondoka pahali mupumbafu anapokuwa, maana pale anapokuwa hakuna maneno ya hekima.
Kwa mupumbafu hekima ni ngumu kuielewa; penye mukutano wa mashauri hafungui mudomo.
Kinywa changu kitasema maneno ya haki, hakuna udanganyifu wala upotevu katika midomo yangu.
Mwenye mazarau hapendi kuonywa, hatafuti hata kidogo maoni ya wenye hekima.
Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?