4 Bila ngombe wa kulima gala za mutu ni tupu. Mavuno mengi yanapatikana kwa nguvu ya ngombe wa kulima.
Shamba la masikini linatoa mazao mengi, lakini linanyanganywa juu ya wale wanaopotosha haki.
Mimi niliwanyima chochote cha kutafuna, nikasababisha ukosefu wa chakula popote. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Ngombe wetu wakuwe na afya na nguvu, kusitokwe mimba wala kukosa kuibeba. Kusikuwe tena kilio katika mitaa yetu.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.
Mushuhuda mwaminifu hasemi uongo, lakini asiyeaminiwa anabubujika uongo.
Utamutegemea kwa sababu ana nguvu nyingi na kumwacha akufanyie kazi zako nzito?