3 Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Anayechunga kinywa chake na ulimi wake, anajiepusha na matatizo.
Ulimi una nguvu ya kuleta uzima na kuua; wanaopenda kuutumia watakula matunda yake.
Kinywa cha mupumbafu kinamwangamiza mwenyewe; mudomo wake ni mutego wa kumunasa yeye mwenyewe.
Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa Yedutuni. Zaburi ya Daudi.
Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.
Mupiga domo hafichi siri. Kwa hiyo umwepuke mutu wa kusemasema.
Kama mutu akizani kwamba yeye ni mutu wa dini naye hawezi kuzuiza ulimi wake, anajidanganya mwenyewe, nayo dini yake haina faida.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Unatamani kufurahia maisha, kuishi maisha marefu na kufurahia mazuri?
Ee Yawe, ulinde kinywa changu, uweke mulinzi kwenye mulango wa kinywa changu.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
Samusoni akamujibu: “Wakinifunga kwa kamba nyipya ambazo hazijatumiwa, nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
hakuweza kuvumilia, akamufunulia siri yake, akisema: “Nywele zangu hazijapata kunyolewa hata kidogo. Mimi nimewekwa Munaziri wa Mungu tangu katika tumbo la mama yangu. Kama nikinyolewa nguvu zangu zitanitoka, nami nitakuwa zaifu kama mutu yeyote.”
Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
Ndani ya kinywa cha mupumbafu kunatokea maneno ya kiburi, lakini mwenye hekima analindwa na maneno yake.