Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 13:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 Mwenye haki yuko na chakula cha kumutoshelea, lakini tumbo la waovu linataabika kwa njaa.

Gade chapit la Kopi




Mezali 13:25
17 Referans Kwoze  

Mumwabudu Yawe, enyi watakatifu wake, maana wenye kumwabudu hawakosewi kitu.


Yawe hawaachi wenye haki wapate njaa, lakini anapinga tamaa za waovu.


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


Wakati ule umasikini utakushambulia kama munyanganyi, ukosefu utakufuata kama mwizi mwenye silaha.


Watakonda kwa njaa, wataangamizwa kwa homa kali. Nitaleta nyama wenye meno makali kuwashambulia, na nyoka wenye sumu wanaotambaa juu ya mavumbi.


Kwa maana, wakati tulipokuwa kwenu, tulikuwa tunawaagiza hivi: “Mutu yeyote asiyetaka kutumika, na hapaswi kula vilevile.”


lakini kumbuka kwamba unapokuwa katika usingizi, umasikini utakufikia kama munyanganyi, ukosefu kama mutu mwenye silaha.


Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.


Umutumainie Yawe na kutenda mazuri, upate kuishi katika inchi na kuwa salama.


Kwa hiyo mutawatumikia waadui zenu ambao Yawe atawatuma mbele yenu, kwa njaa, kiu na uchi, na ukosefu wa kila kitu. Atawafunga nira ya chuma mpaka awaangamize.


Alipokwisha kumaliza mali yake yote, njaa kubwa ikatokea katika inchi ile, akaanza kuishi katika ukosefu.


Anajaza maisha yangu na raha, hata ninabaki kijana mwenye nguvu kama tai.


Nitaubariki Sayuni kwa mahitaji yake; nitawashibisha chakula wamasikini wake.


Umasikini na mazarau vinamupata yule asiyejali mafundisho, lakini mwenye kusikia maonyo anaheshimiwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite