1 Mutoto mwenye hekima anasikia maagizo ya baba yake, lakini mwenye kiburi hasikilizi maonyo.
Mupumbafu anazarau mafundisho ya baba yake, lakini anayekubali maonyo ni mwenye akili.
Mutoto mwenye hekima anamufurahisha baba yake, lakini mupumbafu anamuzarau mama yake.
Hizi ni mezali za Solomono: Mutoto mwenye hekima ni furaha ya baba yake; lakini mutoto mupumbafu ni huzuni ya mama yake.
Mutu akimukosea mwenzake, anaweza kuombewa kwa Mungu, kusudi Mungu amusamehe. Lakini mutu akimukosea Yawe nani anayeweza kumwombea musamaha?” Lakini watoto hao hawakumusikiliza baba yao, maana Yawe alikwisha kata shauri la kuwaua.
Mwenye mazarau anatafuta hekima naye haipati, lakini mwenye akili anapata maarifa kwepesi.
Mwenye mazarau hapendi kuonywa, hatafuti hata kidogo maoni ya wenye hekima.
Alitenda mema mbele ya Yawe kama vile baba yake Asa alivyofanya.
Sasa wana wangu, munisikilize; mutege sikio kwa maneno ya kinywa changu.
Mupumbafu anaona njia yake kuwa sawa, lakini mwenye hekima anasikiliza shauri.