Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 12:2
14 Referans Kwoze  

Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.


Barnaba alikuwa mutu mwema, mwenye kujazwa na Roho Mutakatifu na mwenye imani sana. Na watu wengi wakaongezeka kwa Bwana.


Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.


Ni vigumu kwa mutu kukubali kufa kwa ajili ya mwenye haki. Labda mutu anaweza kujitolea kufa kwa ajili ya mutu mwema.


Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.


Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.


moyo unaopanga mipango miovu, miguu inayokuwa mbio kutenda maovu,


kusudi nitangaze sifa zako mbele ya watu wa Sayuni, nipate kushangilia kwa sababu umeniokoa.


Abusaloma alimwambia: “Maneno yako ni ya haki kabisa. Lakini hakuna mutu yeyote aliyechaguliwa na mufalme kwa kukusikiliza.”


Hivyo utakubaliwa na kusifiwa, mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.


Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.


Anayepanga kutenda maovu kweli anakosa! Wanaopanga kutenda mazuri watapata mema na uaminifu.


Mwenye kuwaka hasira haraka anatenda kipumbafu, lakini mwenye akili ana uvumilivu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite