1 Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.
Azabu kali ni kwa wanaoacha mwenendo mwema; yeyote anayechukia kuonywa atakufa.
Anayejitenga na wenzake anajipendelea mwenyewe; anakasirika akipewa shauri lolote jema.
Matendo yako, ee Yawe, ni makubwa sana! Mawazo yako hayatambulikani!
Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu, ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa, kama sivyo hawatakukaribia.”
Atatumia ubaya wa kila namna kwa kuwadanganya wale wanaopotea kwa sababu hawakupenda kukubali na kupenda mambo ya kweli yaliyoweza kuwaokoa.
Ninawapenda wale wanaonipenda; wanaonitafuta kwa bidii wananipata.
“Sasa basi, wana wangu, munisikilize: heri wale wanaofuata njia zangu.
Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!
Unifundishe namna ya kushika kanuni zako, nami nitafikiri juu ya matendo yako ya ajabu.
Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.
Asiyenipata anajizuru mwenyewe; wote wanaonichukia wanapenda kifo.”
Ikiwa mwenye haki anapata malipo hapa katika dunia, hakika mwovu na mwenye zambi watalipwa!
Mutu muzuri anapata rehema za Yawe, lakini mwenye nia mbaya analaaniwa na Mungu.
Mimi ni mupumbafu sana, wala si mutu; sina akili ya mwanadamu.
Kuhani atamwangalia na kama kivimba cheupe ambacho kimefanya nywele zake zikuwe nyeupe na kivimba kile kimegeuka kuwa kidonda kibichi,
Afazali mutu mwema anipige kwa kunionya; lakini sikubali hata kidogo kusifiwa na wabaya, maana ninaomba siku zote juu ya maovu yao.
Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.