8 Mutu wa haki anaokolewa katika shida, na mwovu anaingia mule kwa pahali pake.
Mwovu atakuwa malipo kwa ukombozi wa wenye haki; nao wasiokuwa waaminifu kwa pahali pa watu wa usawa.
Mwovu akikufa, tumaini lake nalo linatoweka. Tumaini la asiyemwogopa Mungu ni la bure.
Asiyemwogopa Mungu anaangamiza wengine kwa kinywa chake, lakini mwenye haki anaokolewa kwa maarifa yake.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Yawe anawaokoa watu wa haki, na kuwalinda wakati wa taabu.
Mufalme akaamuru wale watu waliomuchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake wao na watoto wao. Nao, hata mbele hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.