25 Mutu anayetoa kwa moyo safi atafanikishwa. Mutu anayekunywesha mwingine maji, naye atakunyweshwa.
Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!
Lakini wenye heshima wanatenda mambo ya heshima, nao wanatetea mambo yenye heshima.
Anayesaidia wamasikini hatakosewa kitu, lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.
Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.
Kwa hiyo gala zako zitajaa ngano, na mitungi yako itafurika na divai mupya.
Kuna watu wanaotoa mali yao kwa wingi na kuzidi; lakini wachoyo wanazilinda na kuendelea katika umasikini.
Muchoyo anachochea magomvi, lakini anayetegemea Yawe atafanikiwa.