21 Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.
Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”
Nitawapa moyo mumoja na nia moja, wapate kuniheshimu mimi siku zote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao watakaofuata.
Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Yawe. Hakika mutu wa namna hiyo hatakosa kuazibiwa.
Siku zote yeye anakopesha kwa moyo safi, na watoto wake ni wenye baraka.
Mutu muzuri anawaachia wazao wake urizi, lakini mali ya mwenye zambi imelundikiwa wenye haki.
Usifuate watu wengi kwa kutenda ubaya. Wala wakati wa kukata maneno, usishuhudie kufuatana na watu wengi kwa kupotosha haki.
Silikasirikii tena shamba hili; kama miiba na michongoma ingelilishambulia, mimi ningepambana nayo na kuichoma kwa moto.
Wenye nia mbaya ni chukizo kwa Yawe, lakini wenye mwenendo mukamilifu ni furaha yake.
Mwanamuke muzuri asiyekuwa na akili ni kama pete ya zahabu kwenye pua la nguruwe.
Kisha, wanaume wote waliojua kwamba wake wao walikuwa wameifukizia miungu mingine ubani, na wanawake wote waliokuwa hapo, kusanyiko kubwa la watu pamoja na Waisraeli waliokuwa wanakaa Patro katika inchi ya Misri walimujibu Yeremia:
Ujitenge mbali na mashitaki ya uongo wala usiwaue wasiokuwa na kosa na wenye haki, maana mimi sitamusamehe mutu mwovu.
Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu, hukumu ya haki imekupata.
Wenye haki hawapatwi na jambo lolote baya, lakini waovu wanapata hasara nyingi.