Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 11:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Anayemuzarau jirani yake hana akili; mutu mwenye ufahamu anakaa kimya.

Gade chapit la Kopi




Mezali 11:12
15 Referans Kwoze  

Wakati walipomutukana, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakutisha watu hata wamwogope. Lakini alijiachilia katika mikono ya Mungu anayehukumu watu kwa haki.


Kwenye kuwa maneno mengi hakukosekani makosa, lakini aneyezuia ulimi wake ana akili.


Vilevile Yesu akawaambia mufano huu kwa ajili ya watu waliojiona kuwa wenye haki na kuwazarau wengine.


Wakati Wafarisayo waliposikia maneno haya yote wakamuzarau Yesu, kwa sababu walikuwa wapenda feza.


Anayemuzarau jirani yake ni mwenye zambi, lakini ana heri yule anayekuwa mwema kwa masikini.


Lakini watu walinyamaza, wala hawakumujibu neno kama vile walivyoamuriwa na mufalme akisema: “Musimujibu.”


Lakini watu wengine wasiofaa kitu, walisema: “Mutu huyu anaweza kutuokoa?” Walimuzarau Saulo na hawakumupa zawadi yoyote. Lakini yeye hakukasirika.


Kisha Zebuli akamwambia: “Majivuno yako yako wapi sasa? Si ni wewe uliyesema: ‘Abimeleki ni nani? Kwa nini tumutumikie?’ Sasa, hao ndio watu uliowazarau. Kwenda upigane nao.”


Anayezini hana akili kabisa; anajiangamiza yeye mwenyewe.


Muji unafanikishwa kwa baraka za watu wa usawa, lakini unaangamizwa kwa kinywa cha waovu.


Anayepitapita akichongea anatoa siri, lakini anayeaminiwa anaficha siri.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite