8 Mwenye hekima anakubali maonyo, lakini mupumbafu anayesemasema mingi ataangamia.
Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.
Nani anayekuwa na hekima na ufahamu kati yenu? Basi aonyeshe jambo lile kwa njia ya mwenendo wake muzuri, kwa njia ya matendo yanayofanyika katika upole unaotokana na hekima ile.
Umufundishe mwenye hekima naye atazidi kuwa na hekima; umufundishe mutu wa haki naye atazidi kuwa na elimu.
Mwenye hekima akizisikiliza, zitamwongezea elimu; na mwenye ufahamu zitamupatia ujuzi.
Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.
Bidii katika kila kazi inaleta faida, lakini maneno matupu yanaleta umasikini.
Hekima ya mwenye akili inamwonyesha njia yake, lakini upumbafu wa wapumbafu unawadanganya wenyewe.
Anayechunga kinywa chake analinda maisha yake, mwenye midomo mirefu anajiletea maangamizi.
Mutu mwovu ananaswa kwa uongo wake mwenyewe, lakini mwenye haki anatoka katika taabu.
Anayekonyeza macho kwa nia mbaya analeta taabu, lakini anayeonya waziwazi analeta amani.
Unieleweshe nipate kushika sheria yako, niifuate kwa moyo wangu wote.
Usimwonye mwenye kiburi maana atakuchukia; umwonye mwenye hekima naye atakupenda.
Wenye hekima wanalinda maarifa, lakini kusemasema kwa mupumbafu kunaleta maangamizi haraka.