5 Mwenye akili anakusanya wakati wa mavuno. Kulala wakati wa kuvuna ni haya.
lakini anajiwekea chakula wakati wa kipwa, anajikusanyia akiba wakati wa mavuno.
siafu ni wadudu wasiokuwa na nguvu, lakini wanajiwekea chakula wakati wa kipwa;
Anayemutesa baba yake na kumufukuza mama yake ni mutoto asiyefaa na mupotovu.
Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.
Muke mwema ni taji la utukufu kwa mume wake. Anayemupatisha mume wake haya ni kama kidonda ndani ya mifupa yake.
Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu, fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.
Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.
Mwenye haki anajiletea baraka yeye mwenyewe, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
Nyuma ya kukata majani, wakati nyasi zinachipuka upya, kusanya majani toka kwenye milima.