26 Kama vile siki inavyokuwa kwa meno au moshi ndani ya macho, ndivyo muvivu anavyokuwa kwa bwana wake.
Kutuma ujumbe kwa mukono wa mupumbafu ni kama kujikata miguu au kujitafutia mateso.
Mujumbe mwaminifu anamufurahia yule aliyemutuma, kama maji ya baridi wakati wa joto la mavuno.
Basi musigeuke kuwa wavivu, lakini mufuate mufano wa wale wanaoamini na kuvumilia. Kwa njia hiyo wanapokea yale Mungu aliyoahidi kuwapa.
Naye bwana wake akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya na muvivu! Ulijua kama ninavuna nafasi nisipopanda, na kukusanya nafasi nisiposambaza.
Kumwimbia mutu mwenye huzuni ni kama kumuvua nguo wakati wa baridi, au kutia siki katika kidonda.
Musikuwe wavivu katika kazi lakini mukuwe na bidii, mukimutumikia Bwana kwa juhudi.
Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.
Ewe muvivu! Kwenda kuchunguza siafu, fikiri juu ya namna yake ya kuishi upate hekima.