Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 10:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Maneno ya mwenye haki yanawafalia watu wengi, lakini wapumbafu wanakufa kwa kukosa akili.

Gade chapit la Kopi




Mezali 10:21
28 Referans Kwoze  

Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?


Pahali zile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia, ni mufano wa watu wanaosikia habari ya Ufalme na kukosa kuielewa. Na kisha yule mwovu Shetani anakuja na kuondoa mbegu zilizopandwa ndani ya mioyo yao.


“Muliyachukia maarifa, wala hamukuchagua kumwogopa Yawe,


Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.


Yeye anakufa kwa ajili ya ukosefu wa mafundisho, anaangamia kwa sababu ya upumbafu wake mukubwa.


Kwa hiyo utasema: “Kwa nini nilichukia mafundisho? Kwa nini nilizarau ndani ya moyo wangu?


Basi, mutakula matunda ya mienendo yenu, mutageukiwa na mashauri yenu wenyewe.


Sijaacha hata kidogo kushika amri yake; maneno yake nimeyatunza ndani ya moyo wangu.


Palepale maneno yako yaliponifikia, niliyameza; nayo yakanifurahisha, yakakuwa matamu katika moyo wangu, maana mimi ninajulikana kwa jina lako, ee Yawe wa majeshi.


Maneno ya ovyo yanaumiza kama upanga, lakini kusema kwa mwenye hekima kunaponyesha kidonda.


Ninawaonya, muchunge lile kundi Mungu alilowapatia, si kwa kulazimishwa, lakini kwa mapenzi yenu sawa vile Mungu anavyotaka. Musitumike kwa ajili ya tamaa mbaya ya mali, lakini kwa kujitoa kwa moyo mwema.


Hivi kufuatana na vile walivyokataa kumutambua Mungu, Mungu akawaacha wafuate akili yao ya upotevu, kusudi wafanye mambo wasiyopaswa kufanya.


Nitawapa wachungaji wanaopendeza moyo wangu, watakaowakulisha kwa akili.


Mutu wa haki anasema maneno ya hekima, kwa ulimi wake anasema kufuatana na sheria ya Mungu.


Mutu muzuri anatwaa vitu vizuri toka ndani ya akiba yake nzuri, naye mutu mubaya anatwaa vitu vibaya toka ndani ya akiba yake mbaya.


Anayezini hana akili kabisa; anajiangamiza yeye mwenyewe.


Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Kwa hiyo, utaweza kulinda akili, na kinywa chako kitashika maarifa.


Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.


Misemo ya wenye hekima ni kama fimbo ya kuongoza ngombe. Mezali zilizokusanywa pamoja na muchungaji mumoja ni kama misumari iliyopigiliwa kwa nguvu.


Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa katika uhamisho kwa sababu ya ukosefu wao wa akili. Wakubwa wao watakufa na njaa, watu wengi watakufa na kiu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite