Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 10:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mali iliyopatikana kwa njia mbaya haifai, lakini haki inaokoa mutu kutoka kifo.

Gade chapit la Kopi




Mezali 10:2
15 Referans Kwoze  

Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Mali inayopatikana kwa udanganyifu ni muvuke unaopita na mutego wa kifo.


Haki ni njia ya uzima, lakini uovu unaongoza katika kifo.


Hivi kama vile zambi ilivyotawala na kuleta kifo, hivi vilevile neema ya Mungu itawale kwa njia ya haki na kuleta uzima wa milele, kwa njia ya Yesu Kristo Bwana wetu.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Watatupa feza yao ndani ya barabara na zahabu yao itakuwa kama kitu kichafu. Feza na zahabu zao hazitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe; wala hawataweza kushiba au kujaza tumbo zao feza na zahabu waliyojilundikia; maana mali hiyo ndiyo iliyosababisha zambi yao.


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


na kuungana naye kabisa. Nami sihesabiwi haki tena kufuatana na mambo niliyofanya, ndiyo ile haki inayopatikana kwa njia ya kushika Sheria. Lakini ninahesabiwa haki kwa njia ya kumwamini Kristo, ndiyo ile haki inatoka kwa Mungu, naye anamuhesabia haki yule anayeamini.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mali ya harakaharaka inatoweka, lakini anayekusanya kidogokidogo ataiongeza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite