11 Kinywa cha mwenye haki ni chemichemi ya uzima, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
Mafundisho ya wenye hekima ni chemichemi ya uzima; inamwezesha mutu kuepuka mitego ya kifo.
Mwenye haki anajiletea baraka yeye mwenyewe, lakini kinywa cha mwovu kimesongwa na mateso makali.
Maneno ya kinywa cha mutu ni kilindi cha maji; chemichemi ya hekima ni kijito kinachobubujika.
Musiseme neno lolote baya, lakini kama ni lazima museme tu maneno mazuri na ambayo yanasaidia kuwajenga wengine na yanayoleta neema kwa wale wanaoyasikia.
Kuna zahabu na wingi wa mawe ya bei kali; lakini kitu cha bei kali zaidi ni maneno ya maarifa!
Mudomo wa mwenye hekima unaeneza maarifa, lakini sivyo kwa mioyo ya wapumbafu.
Midomo ya wenye haki inajua mambo yatakayokubaliwa, lakini vinywa vya waovu vinasema tu maovu.
Watu wa usawa wanapoona jambo hilo wanafurahi, lakini waovu wote wananyamazishwa.
Ulimi mupole ni musingi wa uzima, lakini uovu wake unavunja moyo.