Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mezali 1:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Musikilize maonyo yangu; nitawamiminia mawazo yangu, nitawajulisha maneno yangu.

Gade chapit la Kopi




Mezali 1:23
26 Referans Kwoze  

Basi, uwaambie: Kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– mimi sikifurahii kifo cha mutu mwovu, lakini ninapenda mutu mwovu aachane na mwenendo wake mubaya, apate kuishi. Mugeuke, muachane na mwenendo wenu mubaya, enyi Waisraeli! Kwa nini munataka kufa?


Basi mugeuke toka katika zambi, mumurudilie Mungu, kusudi awasamehe zambi zenu.


Hali itaendelea kuwa hivyo mpaka tujazwe Roho wa Mungu kutoka juu. Hapo jangwa litakuwa shamba lenye udongo muzuri tena, na mashamba yenye udongo muzuri yatakuwa pori.


Lakini kwanza nilihubiri wakaaji wa Damasiki, na wa Yerusalema na wa jimbo lote la Yudea nao watu wa mataifa mengine vilevile. Nilihubiri kwao kwamba wageuke toka zambi zao na kumurudilia Mungu, nao waonyeshe kwa njia ya matendo yao kwamba wamegeuka.


Basi ikiwa ninyi munaokuwa waovu munajua kuwapa watoto wenu vitu vizuri, inaonyesha hakika kwamba Baba yenu anayekuwa mbinguni atawapa Roho Mutakatifu wale wanaomwomba kwake.”


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Anayependa mafundisho anapenda maarifa, lakini asiyependa kuonywa ni mujinga.


Enyi mbingu, munyeshe umande kutoka kule juu, mawingu yatiririshe ushindi; dunia ifuguke, ichipushe wokovu, na kuotesha haki vilevile! Mimi, Yawe nimefanya hayo.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Anayekubali kufundishwa anaelekea kwenye uzima, lakini anayekataa kuonywa amepotoka.


Wimbo wa sifa wa Daudi. Nitakutukuza, ee Mungu wangu na mufalme wangu; nitalitukuza jina lako kwa milele na milele.


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, maana, mimi ndimi Bwana wenu. Nitawatwaa mumoja kutoka kila muji, na wawili kutoka katika kila ukoo, niwapeleke mpaka kwenye mulima Sayuni. –Ni ujumbe wa Yawe.


mulikataa shauri langu, mukazarau maonyo yangu yote.


Maana amri hizi ni taa, na shauri hilo ni mwangaza. Maonyo hayo ya mafundisho ni njia ya uzima.


mumetupilia mashauri yangu yote, mumezarau maonyo yangu.


(Alisema vile juu ya Roho atakayepokelewa na wale wanaomwamini Yesu. Kwa wakati ule Roho alikuwa hajatumwa bado, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa.)


Mutatambua kwamba mimi niko kati yenu, enyi Waisraeli; na kwamba mimi Yawe, ndimi Mungu wenu wala hakuna mwingine. Watu wangu, hawatazarauliwa tena hata kidogo.


Kisha mambo hayo nitashusha Roho wangu juu ya watu wote. Watoto wenu wanaume na wabinti watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite