2 Zitawawezesha watu kujua hekima na mafundisho, na kufahamu misemo yenye maana kubwa.
Uambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”, na Akili: “Wewe ni rafiki yangu”.
Kwa nini mupumbafu kuwa na feza katika mukono kwa kununua hekima, wakati yeye mwenyewe hana akili?
Enyi wajinga, mujifunze kuwa na akili; musikilize kwa uangalifu, enyi wapumbafu.
Kupata hekima ni bora kuliko zahabu; kupata akili ni chaguo bora kuliko feza.
Wana wangu, musikilize maadibisho ya baba yenu, mutege sikio mupate kuwa na akili.
Kumwogopa Yawe ni mafundisho ya hekima; mbele ya kuheshimika inafaa kuwa munyenyekevu.
Ukinisikiliza, utafahamu haki, usawa, na kufuata sheria ya Mungu; utafahamu kila njia nzuri.
Musikilize mafundisho mupate hekima, wala musiyakatae.
Sikiliza shauri na kupokea mafundisho, upate hekima ya kukufaa kwa siku zinazokuja.