Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 9:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Watu walipoona jambo hilo wakaogopa na kumusifu Mungu aliyewapa watu mamlaka ya namna ile.

Gade chapit la Kopi




Matayo 9:8
22 Referans Kwoze  

Watu wote wakashikwa na woga, nao wakamutukuza Mungu, wakisema: “Nabii mukubwa ametokea tena kwetu! Mungu amekuja kuwasaidia watu wake.”


Yale makundi ya watu wakashangaa sana wakati walipowaona wabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanatembea, na vipofu wanaona. Nao wakamusifu Mungu wa Waisraeli.


Kisha wale wakubwa wa baraza wakawakataza tena kwa ukali na kuwaachilia kwenda. Hawakupata njia ya kuwaazibu kwa maana watu wote walikuwa wakimusifu Mungu kwa ajili ya jambo lile lililotendeka.


Mukubwa wa waaskari alipoona mambo yale yaliyotokea, akamusifu Mungu, akisema: “Hakika mutu huyu alikuwa mwenye haki!”


Na mumoja wao alipoona kwamba amekwisha kupona, akarudia akimusifu Mungu kwa sauti kubwa.


Na watu wote walipokuwa wakimwangalia mutu yule, pale pale akasimama, akatwaa kipoyi chake na kujiendea. Wote wakashangaa, wakamusifu Mungu, wakisema: “Hatujaona mambo kama haya hata mara moja!”


Nao yalimusifu Mungu kwa ajili yangu.


Kama mukizaa matunda mengi, Baba yangu atatukuzwa, na hivi mutakuwa kweli wanafunzi wangu.


Halafu akaweka mikono juu yake kwa kumuponyesha. Na mara moja akainuka tena, na kumutukuza Mungu.


Wandugu waamini waliposikia maneno hayo, wakatulia na kumusifu Mungu, wakisema: “Kumbe Mungu amewajalia hata watu wa mataifa mengine vilevile kusudi waweze kugeuka toka zambi na kupata uzima kamili.”


Nao waliposikia maneno hayo, wakamusifu Mungu. Na kisha wakamwambia Paulo: “Ndugu, unaona namna maelfu ya Wayuda walivyoamini; nao wote wanajitolea sana kwa kushika Sheria.


Nao watu wakashangaa sana na kusema: “Mambo anayofanya ni mazuri kweli. Anawawezesha hata viziwi wasikie, nao wabubu wapate kusema.”


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Na kundi lote la watu waliokuwa pale wakashangaa na kusema: “Huyu anaweza kuwa kweli Mwana wa Daudi?”


Vilevile, mwangaza wenu unapaswa kuangaza mbele ya watu, kusudi waone matendo yenu mazuri, nao wamutukuze Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Na mutu yule akasimama na kwenda kwake.


Kisha wachungaji wakarudia wakitukuza Mungu na kumusifu kwa ajili ya mambo yote waliyoyasikia na kuyaona, kwa maana yote yalifanyika sawa vile malaika alivyokuwa amewaambia.


Hakuna mwingine kati yao aliyerudia kwa kumutolea Mungu shukrani, isipokuwa huyu mugeni tu?”


Na pale pale akapata kuona, na kumufuata Yesu akishukuru Mungu. Na watu wote walipoona jambo hili wakamusifu Mungu.


Kufuatana na ushuhuda wa kazi hii, watu watamutukuza Mungu kwa kuona jinsi munavyoonyesha utii wenu katika kushika Habari Njema ya Kristo. Vilevile wanamutukuza kwa kuona moyo wa kutoa munaokuwa nao katika kushirikiana mali yenu pamoja nao na sisi.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite