Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 9:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Na kule wakamuletea mutu mwenye ugonjwa wa kupooza, akilala juu ya kipoyi. Yesu alipoona namna watu wale walivyomwaminia, akamwambia yule mwenye kupooza: “Mutoto wangu, ujipe moyo! Zambi zako zimesamehewa!”

Gade chapit la Kopi




Matayo 9:2
32 Referans Kwoze  

Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.


Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”


Na hata watu walitwaa vitambaa na nguo zilizogusa mwili wa Paulo, wakazipeleka kwa wagonjwa, nao wakapona na pepo wakatoka ndani yao.


Basi Yesu akawauliza: “Watoto wangu, mumepata samaki?” Wakamujibu: “Hapana.”


Yesu aliposikia maneno haya, akashangaa na kuwaambia watu waliomufuata: “Kweli ninawaambia: katika inchi yote ya Israeli, sijaona bado mutu anayekuwa na imani kubwa kama huyu.


Habari zake zikavuma katika inchi yote ya Suria. Wakamuletea watu wote walioteswa na magonjwa mbalimbali na wenye maumivu ya kila namna, wenye pepo, wenye kifafa na wenye kupooza, naye Yesu akawaponyesha.


Wala si ile tu, lakini tunafurahi kwa ajili ya Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo aliyetupatanisha sasa na Mungu.


Yeye alikuwa akisikiliza mahubiri ya Paulo. Paulo akamukazia macho, naye akaona kwamba kiwete yule yuko na imani ya kuweza kuponyeshwa.


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


Basi, ninataka mujue kwamba Mwana wa Mutu yuko na mamlaka ya kusamehe zambi hapa katika dunia.” Kwa hiyo akamwambia yule mutu mwenye kupooza: “Simama, utwae kipoyi chako na uende kwako.”


Na ilipokuwa magaribi, wakamuletea Yesu watu wengi waliokuwa na pepo. Naye akawafukuza wale pepo akiwaamuru kwa neno tu na kuwaponyesha wagonjwa wote.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Naye hakuhitaji kupewa ushuhuda juu ya mutu yeyote, kwa maana yeye mwenyewe alijua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu.


Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani, ugonjwa wako umepona!”


Ilipokuwa magaribi, jua lilipokuwa limekwisha kutua, wakamuletea Yesu watu wote waliokuwa wagonjwa na waliokuwa na pepo.


Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Utusamehe makosa yetu, kama sisi tunavyowasamehe wanaotukosea,


Kitu gani kinachokuwa chepesi kusema: ‘Zambi zako zimesamehewa’, au kusema: ‘Simama, utembee’?


Lakini mara moja Yesu akasema nao, akiwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”


kwa maana wote walimwona na kuogopa sana. Lakini mara moja Yesu akasema nao na kuwaambia: “Mujipe moyo, ni mimi! Musiogope!”


Yesu akasimama na kusema: “Mumwite.” Basi wakamwita yule kipofu na kumwambia: “Ujipe moyo! Simama, anakuita.”


Usiku ule ule Bwana akamutokea Paulo, akamwambia: “Ujipe moyo! Sawa vile ulivyotoa ushuhuda juu yangu hapa Yerusalema, ni vile vile utakavyopaswa kuutoa katika Roma.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite