Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 9:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Nao Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakawaambia wanafunzi wake: “Kwa sababu gani mwalimu wenu anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”

Gade chapit la Kopi




Matayo 9:11
14 Referans Kwoze  

Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Na wakati walimu wa Sheria wa kikundi cha Wafarisayo walipomwona Yesu akikula pamoja na watu wale, wakawauliza wanafunzi wake: “Kwa sababu gani anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Kwa kuwa yeye mwenyewe ni muzaifu, anaweza kuwavumilia wale waliopotoka bila kujua.


Hakika sisi Wayuda wa kizalikio hatuko watu wa mataifa mengine, hao wenye zambi.


Watu wote walioona hayo wakaanza kunungunika wakisema: “Amekwenda kupanga kwa mutenda maovu!”


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Mutu akikuja kwenu, naye asipowafundisha mafundisho haya, musimukaribishe ndani ya nyumba yenu, wala musimusalimie;


Zawadi gani mutapata kutoka kwa Mungu, kama mukiwapenda tu wenye kuwapenda? Hata walipishaji wa kodi wanaokuwa wakorofi wanatendeana vile!


Nyuma Yesu akaikaa kula chakula ndani ya nyumba ya Matayo. Walipishaji wengi wa kodi na watenda mabaya wengine walikuwa wamekuja pale, nao waliikaa kula pamoja na Yesu na wanafunzi wake.


wakisema: “Uliingia ndani ya nyumba ya watu wasiokuwa wa taifa letu na kula chakula pamoja nao!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite