Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Lakini yule mukubwa akamujibu: “Bwana, mimi sistahili kukupokea ndani ya nyumba yangu. Lakini uamuru kwa neno tu na mutumishi wangu atapona.

Gade chapit la Kopi




Matayo 8:8
18 Referans Kwoze  

Kwa neno lake aliwaponyesha, akawaokoa wasiangamie.


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.


anayekuja nyuma yangu. Mimi sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake.”


Simoni Petro alipoona mambo hayo, akapiga magoti mbele ya Yesu na kusema: “Bwana, utoke karibu nami, kwa sababu mimi ni mutu mwenye zambi!”


Mimi ninawabatiza kwa maji kwa kuonyesha kwamba mumegeuka toka zambi zenu. Lakini yule atakayekuja nyuma yangu atawabatiza kwa Roho Mutakatifu na kwa moto. Yeye ni mwenye uwezo kunipita, nami sistahili hata kumuvua viatu.


Mwana wake akamwambia: ‘Baba, nimemukosea Mungu na nimekukosea wewe vilevile. Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako.’


Sababu hii sistahili kuhesabiwa tena sawa vile mwana wako; unihesabu sawa vile mumoja wa watumishi wako.’


Lakini Yoane akamukatalia, akimwambia: “Ni mimi ninayepaswa kubatizwa nawe; namna gani unakuja kwangu?”


Twaa ile fimbo yako, kisha wewe na ndugu yako Haruni mukusanye watu wote pamoja. Halafu, mbele ya macho yao, uambie jiwe linalokuwa mbele ya macho yao litoe maji yake. Utawatoshea maji ndani ya jiwe watu wote na mifugo yao waweze kunywa.


Ee Yawe, unapokea maombi ya muzaifu; unamutia moyo na kumutegea sikio.


Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,


Yesu akamwambia: “Nitakuja kumuponyesha.”


Hata mimi vilevile ni mutu mwenye kuwa chini ya mamlaka ya wakubwa, na tena nina waaskari wengine wanaokuwa chini yangu. Nami nikimwambia mumoja: ‘Kwenda!’, naye anakwenda. Nikimwambia mwingine: ‘Kuja!’, naye anakuja. Na nikimwambia mutumishi wangu: ‘Fanya hivi!’, naye anafanya vile.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite