Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 7:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Siku ile ya hukumu itakapotimia, wengi wataniambia: ‘Bwana, Bwana, sisi hatukutangaza ujumbe wa Mungu? Nasi hatukufukuza pepo kwa jina lako na kufanya maajabu mengi kwa jina lako?’

Gade chapit la Kopi




Matayo 7:22
23 Referans Kwoze  

na kwa sababu hiyo ninapata mateso haya. Lakini sisikii haya kwa ajili ya ile. Maana ninajua ni nani yule niliyemwamini, nami ninahakikisha kwamba anaweza kuchunga kile alichonipa kwa kunilinda mpaka Siku ile ya kurudi kwake.


Tangia sasa nimetayarishiwa zawadi ya ushindi, ndiyo ile taji ya haki, ambayo Bwana anayekuwa Mwamuzi wa haki atakayonipa siku ile ya kurudi kwake. Wala hatanipa mimi peke yangu tu, lakini na wale wote wanaopenda kumwona wakati atakaporudi.


(Yeye hakusema maneno haya kutokana na mawazo yake mwenyewe; lakini kwa maana yeye ndiye aliyekuwa Kuhani Mukubwa mwaka ule, alitabiri kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa la Wayuda.


Anasema yeye aliyesikia maneno ya Mungu, mutu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu, mutu anayeinama uso mpaka chini na kuona wazi.


Lakini ninyi wandugu, hamuko katika giza, kwa hiyo siku ile haitawafikia kwa rafla kama mwizi.


Ninawaambia hakika kwamba kwa Siku ya hukumu muji ule utaazibiwa vikali zaidi kuliko muji Sodoma.”


“Nyuma, hao wengine wakafika, na kuanza kusema: ‘Bwana, bwana, utufungulie!’


“Lakini hakuna mutu anayejua siku ile na saa, hata wamalaika wa mbinguni, hata Mwana, isipokuwa Baba peke yake tu.


“Si kila mutu anayeniita ‘Bwana, Bwana,’ atakayeingia katika Ufalme wa mbinguni, lakini yule tu anayefanya mapenzi ya Baba yangu anayekuwa mbinguni.


Kiburi cha wanadamu kitashushwa, majivuno ya watu yatanyenyekezwa, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Macho yenye kiburi ya wanadamu yatanyenyekezwa, watu wenye majivuno watashushwa chini, na Yawe peke yake atatukuzwa siku hiyo.


Bwana amusikilie huruma kwa Siku ile! Unajua vizuri sana vilevile mambo yote aliyonitendea kule Efeso.


atakapokuja apate kutukuzwa na watu wake na kushangiliwa na wale wote wanaoamini. Ninyi vilevile mutakuwa pamoja nao kwa maana mumeamini habari tuliyowatangazia.


Kweli ninawaambia: kwa Siku ya hukumu, watu wa muji ule wataazibiwa vikali zaidi kuliko watu wa muji wa Sodoma na wa Gomora.


Kati ya watu hao waliouawa, kulikuwa wafalme watano wa Midiani: Ewi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile wakamwua Balamu mwana wa Beori.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite