Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Mutawatambua kwa matendo yao. Watu hawachumi matunda ya mizabibu au ya tini toka juu ya miti ya miiba.

Gade chapit la Kopi




Matayo 7:16
10 Referans Kwoze  

Wandugu zangu, muti unaotoa matunda ya tini unaweza kutoa matunda ya muzeituni? Au muzabibu unaweza kutoa matunda ya tini? Hapana! Hivi vilevile kisima kinachotoa maji ya chumvi hakiwezi kutoa maji matamu.


“Muti ukiwa muzuri, matunda yake yatakuwa mazuri vilevile; nao muti ukiwa mubaya, matunda yake yatakuwa mabaya vilevile. Kwa maana muti unatambulikana kwa matunda yake.


Basi kwa hiyo, mutawatambua manabii wa uongo kwa njia ya matendo yao.


Yawe aamue kati yangu na wewe. Naye ndiye akulipize kisasi lakini mimi sitanyoosha mukono wangu juu yako hata kidogo.


Hata mutoto anajulikana kwa matendo yake, kama ni safi na sawa.


Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fazili, uaminifu,


Lakini mutu anaweza kusema: “Wewe uko na imani, na mimi niko na matendo.” Mimi nitajibu: “Unionyeshe imani yako pasipo matendo, na mimi nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite