Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 “Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.

Gade chapit la Kopi




Matayo 7:12
19 Referans Kwoze  

Muwatendee wengine sawasawa munavyotaka wawatendee ninyi vilevile.


Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo juu ya wazao wa watu wako lakini umupende mwenzako kama vile unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ni Yawe.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Shabaha ya agizo hilo ni kusudi kuwe upendo unaotokana na moyo safi na zamiri nzuri na imani ya kweli.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Kama mutu mwovu akiachana na zambi zake zote alizotenda, kama akishika masharti yangu yote, na kutenda mambo ya haki na ya ukweli, huyo hakika ataishi, hatakufa.


“Musizani kama nilikuja kuvunja Sheria ya Musa au mafundisho ya manabii. Mimi sikukuja kuvunja, lakini kukamilisha.


Munafanya vizuri kama mukitimiza sheria hii ya kifalme inayopatikana katika Maandiko Matakatifu: “Umupende mwenzako kama unavyojipenda wewe mwenyewe.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite