Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.

Gade chapit la Kopi




Matayo 6:6
17 Referans Kwoze  

Basi, akafunga mulango na kumwomba Yawe.


Kisha kuagana nao, akapanda kwenye kilima peke yake kwa kuomba. Na giza lilipoingia, alikuwa angali kule peke yake,


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Petro akawaamuru watu wote waende inje, akapiga magoti na kuomba. Kisha akaelekea ile maiti na kusema: “Tabita, simama!” Halafu Tabita akafungua macho, na wakati alipomwona Petro akaamuka na kuikaa.


Mukuje watu wangu, muingie ndani ya nyumba zenu, mujifungie humo ndani. Mujifiche kwa muda mufupi, mpaka kasirani ya Yawe ipite.


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


kusudi usijionyeshe kwa watu kwamba unafunga. Jambo hilo litajulikana tu kwa Baba yako anayekuwa kwa siri. Naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


Kesho yake karibu na saa sita ya muchana, hao watu watatu wakafika karibu na Yopa, saa ile Petro akapanda juu ya paa kwa kuomba.


Hivi tendo lile halitatoka inje, naye Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa.


Kwa sababu hiyo ninapiga magoti mbele ya Baba Mungu,


Kwa maana wale wanaoishi kwa kufuatana na hali ya kimwili, wanashugulika na mambo yanayotakiwa na mwili lakini wale wanaoishi kufuatana na uongozi wa Roho wa Mungu wanashugulika na mambo yanayotakiwa na Roho yule.


Kornelio akajibu: “Kumekwisha kupita siku tatu, mimi nilikuwa nikiomba ndani ya nyumba yangu kwa saa hii hii ya saa tisa ya muchana. Mara moja nikaona mutu anayevaa nguo yenye kungaa sana, akisimama mbele yangu.


Natanaeli akamwuliza: “Unanijua namna gani?” Yesu akamujibu: “Filipo alipokuwa hajakuita, nilikuona wakati ulipokuwa chini ya muti wa matunda ya tini.”


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Hivyo utamufezehesha, kama vile kumwanga makaa ya moto juu ya kichwa chake. Yawe atakupa zawadi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite