Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Matayo 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 “Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.

Gade chapit la Kopi




Matayo 6:5
34 Referans Kwoze  

“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Lakini yule mulipishaji wa kodi alisimama kwa mbali, naye hakusubutu hata kuinua macho yake kuelekea mbingu; lakini alijipigapiga kwa huzuni na kusema: ‘Ee Mungu, unisamehe mimi mutenda mabaya.’ ”


Na munaposimama kwa kuomba, mukiwa na neno na mutu mwingine, mumusamehe, kusudi Baba yenu anayekuwa mbinguni, awasamehe vilevile makosa yenu. [


Kwa hiyo mutakapokuja kunililia na kuniomba, nitawasikiliza.


Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.


Wananyanganya mali ya wajane na kuomba maombi marefu kusudi waonekane mbele ya watu. Kwa sababu hii watahukumiwa vikali sana!”


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Halafu Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu kwa kuwaonyesha kwamba wanapaswa kuomba siku zote pasipo kuchoka.


Hivyo, mufalme Dario akatia sahihi kwenye sheria hiyo.


Mumwombe Mungu kila wakati mukiongozwa na Roho. Mumwombe na kumusihi kwa kila namna. Kwa hiyo mukeshe bila kuchoka mukiwaombea watu wote wa Mungu.


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munapenda kuikaa katika viti vya mbele ndani ya nyumba ya kuabudia na kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi za makutano.


Na kitu chochote mutakachoomba, mukiamini, mutakipata.”


Lakini mimi ninamulilia Mungu, naye Yawe ataniokoa.


Ee Yawe, usikilize maneno yangu, usikie malalamiko yangu.


Mpaka sasa hamujaomba kitu kwa jina langu. Muombe, nanyi mutapewa, na furaha yenu itakuwa kubwa kabisa.


Katika mafundisho yake aliwaambia: “Mujiepushe na walimu wa Sheria, wanaopenda kujitembeza wakivaa kanzu ndefu, na kusalimiwa kwa heshima kwenye nafasi ya makutano.


Basi muombe Bwana mwenyeji wa mavuno awatume wavunaji wengine kwa kuvuna mavuno yake.”


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Yawe. Hakika mutu wa namna hiyo hatakosa kuazibiwa.


Wanapenda kuikaa kwenye nafasi za heshima katika karamu na katika viti vya mbele ndani ya nyumba za kuabudia.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Mujiangalie musifanye matendo mema mbele ya watu kusudi mujionyeshe kwao. Kwa maana mukifanya hivi hamutapata faida kutoka kwa Baba yenu anayekuwa mbinguni.


Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.


Lakini ole kwenu ninyi munaokuwa watajiri, maana hamutapata raha ingine.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite